Geita Gold

Geita Gold yapania robo fainali kombe la FA

Joel JJ By Joel JJ
β€’
1 Mar 2023
Geita Gold yapania robo fainali kombe la FA

Kocha Msaidizi wa Geita Gold FC, Mathias Wandiba, amesema nguvu na akili zao wanazielekeza katika mchezo wa hatua ya 16 bora wa Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) maarufu FA Cup dhidi ya Green Warriors Ijumaa wiki hii

Mechi hiyo itapigwa uwanja wao wa nyumbani wa Nyakumbo, uliopo mkoani humo, wakiwakaribisha 'Wajeda' hao wa Ligi ya Championships, ambao maskani yao ni Dar es Salaam.

Wandiba alisema wamerejea nyumbani wakitokea Ruangwa baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 ugenini katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Namungo FC.

Alisema wanaendelea na maandalizi kwa kufanyia kazi madhaifu yaliyojitokeza katika mechi iliyopita na kujiimarisha kwa mchezo ujao wa Kombe la Shirikisho la Azam.

"Maandalizi yanaendelea vizuri kwani ni mchezo uko kwenye ratiba kama ilivyo mechi zingine za ligi na wachezaji watakaokosekana kwa sasa hadi tupate ripoti ya daktari wa timu," alisema Wandiba.

Alisema hawana mpango wa kufanya mabadiliko ya kikosi katika mchezo huo na kwamba hilo linaweza kutokea endapo tu watapata ripoti ya daktari wa timu hiyo kutokana na kugundulika watawakosa baadhi ya wachezaji kwa sababu ya majeraha.

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
18h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
21h ago
READ MORE β†’