Yanga yaifumua Prisons 4-1

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd March 2023


Yanga yaifumua Prisons 4-1

Yanga imetinga robo fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) baada ya ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Tanzania Prisons katika mchezo ulipigwa uwanja wa Azam Complex

Ulikuwa mchezo uliotawaliwa na Yanga kwa muda mwingi lakini hadi mapumziko hakukuwa na mabao kutoka kila upande licha ya Yanga kufanya majaribio mengi zaidi kwenye lango la Prisons

Hata hivyo Yanga ilirejea ikiwa na kasi zaidi kwenye kipindi cha pili, alikuwa nahodha Bakari Nondo Mwamnyeto aliyeitanguliza Yanga kwa bao la mapema kwenye kipindi cha pili kabla ya Jumanne Elifadhili hajasawazisha kupitia mpira wa kichwa

Kuingia kwa bao hilo kuiifanya Yanga iongeze kasi ya mashambulizi na kufanikiwa kufunga mabao mengine matatu kupitia kwa Clement Mzize aliyefunga mabao mawili pamoja na Stephane Aziz Ki aliyefunga kupitia mkwaju wa penati

Mzize angeondoka na mpira leo kama angefunga mkwaju wa penati kwenye dakika za majeruhi

Mzize anaongoza mbio za ufungaji bora akiwa amefikisha mabao sita

Mchezo huo ulishuhudiwa na Mwenyekiti wa Makampuni ya GSM, Ghalib Said Mohammed

Aidha klabu ya Singida Bi Stars imetinga robo fainali baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania wakati Geita Gold nao wakitinga robo fainali kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Green Worriors


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.