Wahuni washambulia duka la mke wa Messi Argentina

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th March 2023


Wahuni washambulia duka la mke wa Messi Argentina

Polisi huko Argentina linawatafuta watu wawili wenye silaha walioshambulia duka la mke wa mshambuliaji wa Argentina, Lionel Messi, Antonela Roccuzzo (35) jijini Rosario, nchini humo

Tukio hilo limeripotiwa kutokea mapema Ijumaa alfajiri baada ya watu wawili waliokuwa kwenye pikipiki kufyatua takriban risasi 14 kwenye madirisha ya duka hilo na kuacha ujumbe uliosemeka:

"Messi tunakusubiri wewe, Javkin ni muuza madawa ya kulevya, hatokusaidia"

Kwa mujibu wa taarifa ya Polisi hakuna aliyejeruhiwa katika eneo la tukio ingawa kulikuwa na uharibifu uliofanyika kwenye duka hilo.

Pablo Javkin ambaye ni Meya wa Rosario ameripotiwa kufadhaishwa na tukio hilo huku akisema jambo hilo limeleta ongezeko la ghasia na wasiwasi jijini humo

Mpaka sasa, Messi pamoja na mke wake Antonela Roccuzzo hawajazungumzia tukio hilo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.