Mashabiki wa Yanga Jumapili hii Wameshiriki Wananchi jogging kujiweka sawa kuelekea mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Real Bamako ambao utapigwa Jumatano, March 08 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Jogging hiyo ilianzia Makao Makuu ya Yanga, Jangwani, ikapita Magomeni, Kigogo na kisha kurejea tena Jangwani
Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema Wananchi wanaweka afya sawa ili kuhakikisha siku ya Jumatano wanashusha Full Shangwe pale uwanja wa Benjamin Mkapa






