Mashabiki Yanga waifanyia mazoezi Real Bamako

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th March 2023


Mashabiki Yanga waifanyia mazoezi Real Bamako

Mashabiki wa Yanga Jumapili hii Wameshiriki Wananchi jogging kujiweka sawa kuelekea mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Real Bamako ambao utapigwa Jumatano, March 08 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Jogging hiyo ilianzia Makao Makuu ya Yanga, Jangwani, ikapita Magomeni, Kigogo na kisha kurejea tena Jangwani

Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema Wananchi wanaweka afya sawa ili kuhakikisha siku ya Jumatano wanashusha Full Shangwe pale uwanja wa Benjamin Mkapa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.