Arsenal wanaonyesha dhamira yao ya kuutaka ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Bournemouth hapo jana
Ilikuwa mechi ngumu kwa Arsenal ambao walikuwa nyuma kwa mabao 2-0 kabla ya kusawazisha na kufunga bao la ushindi kwenye dakika za jioniii
Reis Nelson ndiye aliyekuwa shujaa wa Arsenal akifunga bao la ushindi kwenye dakika ya mwisho ya nyongeza (97')
Mapema Manchester City ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Newcastle United na kupunguza tofauti ya alama baina yake ya Arsenal kuwa mbili
Lakini ushindi wa Arsenal umerufisha gap hilo kuwa alama tano huku kila timu ikiwa imeshuka dimbani mara 26
Arsenal ina alama 63 wakati Manchester City ina alama 58, vita hii itaamuliwa katika mechi 12 zilizobaki
Leo saa 1:30 usiku Liverpool itakuwa nyumbani kuumana na Manchester United katika mchezo ambao kama Liverpool watashinda basi watafufua matumaini ya kuwania nafasi nne za juu
Baada ya Spurs kuchapwa 1-0 na Wolves, wamesalia na alama 45 wakiwa wamecheza mechi 26
Liverpool wana alama 39 wakiwa wamecheza mechi 24



