Arsenal wakomaa kileleni EPL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th March 2023


Arsenal wakomaa kileleni EPL

Arsenal wanaonyesha dhamira yao ya kuutaka ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu baada ya ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Bournemouth hapo jana

Ilikuwa mechi ngumu kwa Arsenal ambao walikuwa nyuma kwa mabao 2-0 kabla ya kusawazisha na kufunga bao la ushindi kwenye dakika za jioniii

Reis Nelson ndiye aliyekuwa shujaa wa Arsenal akifunga bao la ushindi kwenye dakika ya mwisho ya nyongeza (97')

Mapema Manchester City ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Newcastle United na kupunguza tofauti ya alama baina yake ya Arsenal kuwa mbili

Lakini ushindi wa Arsenal umerufisha gap hilo kuwa alama tano huku kila timu ikiwa imeshuka dimbani mara 26

Arsenal ina alama 63 wakati Manchester City ina alama 58, vita hii itaamuliwa katika mechi 12 zilizobaki

Leo saa 1:30 usiku Liverpool itakuwa nyumbani kuumana na Manchester United katika mchezo ambao kama Liverpool watashinda basi watafufua matumaini ya kuwania nafasi nne za juu

Baada ya Spurs kuchapwa 1-0 na Wolves, wamesalia na alama 45 wakiwa wamecheza mechi 26

Liverpool wana alama 39 wakiwa wamecheza mechi 24


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.