Mshambuliaji wa PSG Kylian Mbappe amefikia mafanikio mengine katika maisha yake, akimpita Edinson Cavani kama mfungaji bora wa muda wote wa Paris Saint-Germain na bao lake la 201 dhidi ya Nantes kwenye Ligue 1 Jumamosi
Fowadi huyo wa Ufaransa aliifungia PSG bao la nne dakika za lala salama na kupata ushindi wa 4-2 na kuweka rekodi hiyo
Klabu iliandaa hafla fupi baada ya mchezo kumalizika, na picha kubwa ya Mbappe ikionyeshwa kwenye Parc des Princes
"Ni jambo la kipekee sana kuwa hapa. Mara ya mwisho nilipokuwa hapa ilikuwa ni kutangaza kubaki (kuongeza mkataba), ni heshima kuwa hapa kama mfungaji bora wa klabu," alisema Mbappe
"Ni bahati kuwa mchezaji wa PSG, kucheza katika jezi hii ya kihistoria, kwa klabu kubwa nchini Ufaransa"
Mbappe, 24, ameifikia rekodi ya Cavani katika mechi chache sana. Wakati raia huyo wa Uruguay alichukua mechi 301 kufikisha mabao 200, Mbappe alihitaji mabao 247 pekee.
Mzaliwa wa Paris, Mbappe alijiunga na PSG kutoka Monaco mwaka 2017 kwa ada ya uhamisho iliyovunja rekodi ya Euro milioni 180



