Simba - Vipers

Vipers Fc kutua Jumatatu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
5 Mar 2023
Vipers Fc kutua Jumatatu

Wapinzani wa Simba katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika, Vipers Fc kutoka nchini Uganda wanatarajia kuwasili nchini kesho Jumatatu Machi 6 ,2023 kwa ajili ya mchezo dhidi ya Simba utakaochezwa siku ya Jumanne ya Machi 7-2023 kwenye dimba la Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema Vipers Fc wamethibitisha kuingia nchini mapema Jumatatu ambapo siku hiyo jioni watakuwa na ruksa ya kufanya mazoezi kwenye uwanja wa Mkapa majira ya saa 1 usiku

Mgeni rasmi wa mchezo huo ni Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma

Simba inahitaji ushindi ili kujiweka katika nafasi nzuri katika mkakati wa kuisaka hatua ya robo fainali

Kimahesabu bado timu zote zina nafasi ya kusonga mbele hatua inayofuata katika kundi C pamoja na kuwa Raja Casablanca wao wana nafasi nzuri zaidi

Raja ndio vinara wa kundi C wakikusanya alama tisa baada ya kushinda mechi zote tatu wakati Horoya Ac inashika nafasi ya pili ikiwa na alama nne

Horoya wametofautiana alama moja tu na Simba iliyo nafasi ya tatu ikiwa na alama tatu. Vipers Fc wanaburuza mkia wakiwa na alama moja

Mechi za raundi ya nne zinaweza kutoa taswira ya nafasi ya Simba kuelekea robo fainali, lakini ushindi ndio matokeo pekee ambayo Simba inahitaji ili kuwa na matumaini

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
8h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
9h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
9h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
12h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
16h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
17h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
17h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
18h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
18h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
19h ago
READ MORE β†’