Welsey Fofana jana alifunga bao pekee la Chelsea walipoibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Leeds na kumpunguzia presha kocha wa timu hiyo Graham Potter
Ulikuwa ushindi wa pili katika mechi 15 zilizopita, ilikuwa lazima kwa Chelsea kupata ushindi kumpunguzia presha kocha wao Potter licha ya mwenyewe kusisitiza kabla ya mchezo kuwa anaungwa mkono na wamiliki wa klabu
Chelsea wanasalia katika nafasi ya 10 licha ya ushindi huo huku Leeds wakiwa nafasi ya 17 na pointi moja juu ya eneo la kushushwa daraja.
Pamoja na ushindi huo bado mashabiki wa Chelsea hawaonyeshi kuwa na imani na Potter
Usajili mkubwa uliofanywa hauendani na matokeo ambayo Chelsea wameyapata kabla ya ushindi dhidi ya Leeds
Hata hivyo ushindi huo unaweza kuwaongezea morali kupambana katika mechi zilizosalia



