Mshambuliaji Mtanzania Mbwana Samatta leo ameiongoza timu yake ya KRC Genk kupata sare ya mabao 2-2 dhidi ya St Truiden katika mchezo ambao Genk walikuwa ugenini
Samatta alifunga mabao hayo kwenye kila kipindi huku St Truiden wakilazimika kusawazisha mara mbili kupitia kwa Shinji Okazaki na Gianni Bruno
Ni matokeo ambayo yameendelea kuiweka KRC Genk kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na alama 67 baada ya mechi 28
Union Saint Gilloise inashika nafasi ya pili ikiwa na alama 57 baada ya mechi 27
Msimu huu Samatta ameifungia Genk mabao manne katika mechi 23 alizocheza



