Samatta apiga mbili Genk ikipata sare ugenini

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th March 2023


Samatta apiga mbili Genk ikipata sare ugenini

Mshambuliaji Mtanzania Mbwana Samatta leo ameiongoza timu yake ya KRC Genk kupata sare ya mabao 2-2 dhidi ya St Truiden katika mchezo ambao Genk walikuwa ugenini

Samatta alifunga mabao hayo kwenye kila kipindi huku St Truiden wakilazimika kusawazisha mara mbili kupitia kwa Shinji Okazaki na Gianni Bruno

Ni matokeo ambayo yameendelea kuiweka KRC Genk kileleni mwa msimamo wa ligi ikiwa na alama 67 baada ya mechi 28

Union Saint Gilloise inashika nafasi ya pili ikiwa na alama 57 baada ya mechi 27

Msimu huu Samatta ameifungia Genk mabao manne katika mechi 23 alizocheza


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.