Salah mfungaji bora wa muda wote Liverpool

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th March 2023


Salah mfungaji bora wa muda wote Liverpool

Mshambuliaji wa Liverpool raia wa Misri Mohammed Salah ameweka rekodi ya kuwa mchezaji aliyefunga magoli mengi katika Ligi Kuu ya Uingereza katika klabu ya Liverpool baada ya kufikisha mabao 129

Rekodi hii ilikuwa inashikiliwa na Robbie Fowler kwa muda mrefu akifunga mabao 127

Kabla ya mchezo dhidi ya Manchester United hapo jana ambapo Liverpool iliibuka na ushindi wa mabao 7-0,  Salah alikuwa na magoli 127,baada ya kufunga magoli mawili amefikisha magoli 129

Salah amekuwa na mwenendo mzuri wa kupachika mabao akitwaa tuzo ya ufungaji bora ligi ya Uingereza mara tatu

Msimu huu Salah amefunga mabao 19 katika michuano yote, mabao 11 kwenye ligi kuu na mabao nane kwenye michuano ya ligi ya mabingwa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.