Simba

Simba imekamilisha maandalizi kuikabili Vipers Fc

Joel JJ By Joel JJ
6 Mar 2023
Simba imekamilisha maandalizi kuikabili Vipers Fc

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema maandalizi kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Vipers Fc yamekamilika

Robertinho amesema wanatarajia mchezo utakuwa mgumu katika hatua hii lakini wao wanahitaji kutumia vyema uwanja wa nyumbani kushinda

"Tunatarajia mchezo mgumu siku ya kesho lakini sisi tumejipanga kwa ajili kutafuta ushindi. Katika hatua hii hakuna mchezo rahisi kila timu inashuka uwanjani kutafuta matokeo mazuri"

"Tumejiandaa vyema kucheza hapa nyumbani, tunafahamu ubora wa Vipers uko wapi hivyo tutakuwa makini hasa kwenye mashambulizi ya kushitukiza"

"Tayari nimeshaamua timu ambayo itashuka uwanjani kesho lakini siwezi kuweka hadharani hapa. Muhimu ni kuwa wachezaji wangu wako tayari, wana ari na morali kubwa kuelekea mchezo huo," alisema Robertinho

Nae nahodha Msaidizi wa Simba Shomari Kapombe amesema wachezaji wote wako tayari kwa mchezo huo ambao wanahitaji kushinda

"Uzuri sisi kama wachezaji tunafahamu majukumu yetu, tunarejea katika uwanja wa nyumbani tukiwa na lengo moja tu kushinda. Tunajua katika mchezo uliopita hatukufanya vizuri lakini kesho tunarudi tukiwa imara na malengo makubwa ya ushindi"

"Tutafuata maelekeo ambayo Mwalimu ametuandalia kwa kuzingatia ubora wa Vipers Fc. Tumejiandaa vizuri kupata ushindi katika mchezo wa kesho lakini nawaomba mashabiki wa Simba waje kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa, wingi wao utatuongezea morali ya kupambana katika mchezo huo," alisema Kapombe

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
3h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
4h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
6h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
6h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
7h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
7h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
7h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
7h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
8h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
10h ago
READ MORE →