Arsenal

Arteta aota ubingwa Arsenal

Joel JJ By Joel JJ
6 Mar 2023
Arteta aota ubingwa Arsenal

Mkufunzi wa Arsenal Mikel Arteta alisifu bao la ushindi la Reiss Nelson katika dakika ya 97 dhidi ya Bournemouth  kwenye Uwanja wa Emirates akiamini ushindi wa mabao 3-2 waliopata unapaswa kuwapa Arsenal imani zaidi ya kuweza kushinda taji la Ligi Kuu England

Arsenal walikuwa nyuma kwa mabao 2-0 Bournemouth wakifunga kupitia kwa Philip Billing na Marcos Senesi

Hata hivyo, Thomas Partey aliifungia Arsenal kwenye dakika ya 62 kabla ya Ben White kusawazisha dakika nane baadaye

Katika dakika za majeruhi, Nelson alipiga shuti kali kutoka nje kidogo ya 18 na kuipatia timu yake ushindi muhimu uliorejesha tofauti ya poniti dhidi ya wapinzani wao Manchester City kuwa tano

"Labda ni wakati wa furaha zaidi ambao tumekuwa nao," alisema Arteta, ambaye aliteuliwa kuwa kocha wa Arsenal Desemba 2019.

"Safari ambayo tumekuwa pamoja na jinsi mashabiki na wachezaji wanavyojituma, nadhani tuko katika nyakati bora sana"

Tangu kufungwa na Man City Februari 15, mwaka huu, Arsenal imeifunga Aston Villa, Leicester City, Everton na Bournemouth.

"Kushinda mechi nne kwenye Ligi Kuu ni ngumu sana na tumecheza mechi tatu ndani ya wiki, ambayo ni ngumu zaidi"

"Nafikiri pamoja na changamoto ambazo tunaweza kupitia, tunapaswa kuwa na imani zaidi tunaweza kutimiza malengo yetu msimu huu," aliongeza Arteta

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
2h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
6h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
7h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE →
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
8h ago
READ MORE →
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
9h ago
READ MORE →
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
9h ago
READ MORE →
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE →
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE →