Wakati kiungo Feisal Salum akitua Ofisi za TFF mapema leo kuliomba Shirikisho livunje mkataba wake na klabu ya Yanga, uongozi wa klabu hiyo umemuandikia barua kumtaka aripoti kambini haraka
Kulingana na Taarifa kwa UMMA iliyotolewa na Yanga leo, klabu hiyo imeeleza kupokea Maamuzi ya Marejeo ya shauri linalomuhusu Feisal na hivyo kumuandikia barua mchezaji huyo arejee mazoezini kutekeleza matakwa ya mkataba wake ambao unamalizika May 30 2024
Kataika taarifa hiyo, Yanga imeeleza kuwa tayari kujadiliana na Feisal kwa ajili ya kuboreshea maslahi yake huku pia wakiwa tayari kumruhusu mchezaji huyo aondoke kwa kuzingatia sheria za uhamisho za TFF na FIFA
Kwa timu inayohitaji hudumu ya mchezaji huyo imetakiwa kufika mezani kwa ajili ya majadiliano




