Michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika leo inaingia raundi ya nne kwa mechi kadhaa kupigwa
Nchini Tanzania klabu ya Simba itakuwa uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili Vipers Fc katika mchezo wa kundi C utakaopigwa saa 1 usiku
Baada ya ushindi wa bao 1-0 waliopata kule Uganda, Simba wanahitaji kushinda tena leo ili kuweka hai matumaini ya kufuzu hatua ya robo fainali
Vipers Fc inayoburuza mkia kundi C ikiwa na alama moja, kimahesabu pia inaweza kuwa na nafasi kama itashinda siku ya leo
Ni mechi inayotarajiwa kuwa na ushindani mkali ikitarajiwa kushuhudiwa na mashabiki wengi wa Simba
Mechi nyingine zinazopigwa leo, Al Hilal watakuwa nyumbani kuikabili Cotton Sport (1600H), CR Beluizdad vs El Merreikh (2200H), Zamalek vs Esperance (2200H) na Horoya vs Raja (2200H)



