Yanga

Nabi ataka ushindi dhidi ya Real Bamako Jumatano

Joel JJ By Joel JJ
β€’
7 Mar 2023
Nabi ataka ushindi dhidi ya Real Bamako Jumatano

Kocha Mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Real Bamako ambao utapigwa kesho Jumatano katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Nabi amesema wanahitaji kushinda mchezo huo pamoja na mchezo utakaofuata dhidi ya US Monastir ili kuwa na nafasi nzuri ya kutinga robo fainali

Nabi amesema mchezo wa mwisho ambao watacheza ugenini dhidi ya TP Mazembe utakuwa mgumu sana hivyo wanapaswa kutumia vyema uwanja wa nyumbani kukusanya alama sita katika mechi mbili za nyumbani wakianza na Real Bamako

"Tunacheza na timu ambayo tumetoka kucheza nayo Mali. Baada ya Bamako tutacheza na Monastir. Ni mechi ngumu lakini tunahitaji kushinda mechi hizi kwani mechi ya Mazembe itakuwa ngumu zaidi"

"Mechi dhidi ya Real Bamako itakuwa ngumu lakini tumejiandaa, tuko vizuri tutapambana ili tupate ushindi"

"Wachezaji hata sisi makocha hatukufurahia matokeo tuliyopata Mali, tuliumia Real Bamako kusawazisha dakika za mwisho, wachezaji wameahidi kupambana kupata ushindi mnono hapo kesho"

"Tunafahamu Real Bamako hawakuja kufanya utani hivyo tunajua mechi itakuwa ngumu lakini tutajitahidi tupate ushindi," alisema Nabi

Nabi alibainisha kuwa winga Jesus Moloko alipata majeraha kwenye mchezo wa kombe la FA dhidi ya Tanzania Prisons, atafanyiwa tathmini ya mwisho baada ya mazoezi ya leo

"Pia tunasikitika kumkosa Salum Abubakar ambaye amefiwa na mtoto wake leo," alisema Nabi

Aidha Nabi amesema wamefanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza katika mechi zilizopita hasa kwenye mipira ya kona

"Ni kukosa umakini na wachezaji kutokuwa na mawasiliano imepelekea kuruhusu mabao manne ya aina moja katika mechi zilizopita. Jambo hili halihusiani na vimo vya wachezaji, tumefanyia kazi, naamini wachezaji wangu wataongeza umakini katika kukabiliana na mipira inayotokana na kona au faulo"

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
10h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
17h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
18h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
19h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
21h ago
READ MORE β†’