Bruno Fernandes hapaswi kuwa nahodha wa Manchester United kufuatia kipigo cha aibu cha 7-0 Jumapili kutoka kwa Liverpool, anasema Chris Sutton, mchezaji wa zamani wa Chelsea na England.
Mreno huyo, ambaye anakaimu nafasi ya nahodha wa klabu hiyo badala ya Harry Maguire, alikosolewa kwa tabia na mtazamo wake katika mchezo huo.
"Kuna watu ambao wamehitimu zaidi kuwa nahodha, Fernandes sio kiongozi wao bora. kuna wanaofaa zaidi yake, Casemiro akiwa mmoja. Nadhani hapaswi kamwe kuvaa kitambaa tena kwa Manchester United" Sutton aliiambia BBC
Fernandes, mwenye umri wa miaka 28, ana mabao 57 na asisti 50 katika mechi 166 alizoichezea klabu hiyo katika michuano yote, lakini lugha yake ya mwili Anfield iliitwa 'fedheha' na nahodha wa zamani wa United Roy Keane
Nahodha mwingine wa zamani Gary Neville alisema mchezaji huyo anaaibisha nyakati
Katika mchezo huo pia Fernandez alionekana kumsukuma msaidizi wa mwamuzi katika dakika ya 81. Hakuna hatua iliyochukuliwa na mwamuzi wakati huo na tukio hilo halichunguzwi na Chama cha Soka