Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imemtambulisha Adel Amrouche kuwa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' kwa mkataba wa miaka mitatu
Juzi Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) lilimtangaza Amrouche kuwa Kocha Mkuu wa Stars ambapo leo amesaini Mkataba mbele ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Balozi Dkt.Pindi Chana na hivyo kufanyiwa utambulisho rasmi
Serikali ndio iliyomuajiri Kocha huyo na italipa gharama zote katika kipindi chote cha mkataba wake
Amrouche atasaidiwa na Hemed Morocco kama Kocha Msaidizi sambamba na makocha wengine ambao atakuja nao






