PSG - Bayern - Tottenham - Brugge - Chelsea - Ac Milan

Mbappe anaweza kuibeba PSG mbele Bayern leo?

Joel JJ By Joel JJ
β€’
8 Mar 2023
Mbappe anaweza kuibeba PSG mbele Bayern leo?

Michuano ya hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa inaendelea leo, Benfica na Chelsea walitinga robo fainali jana na leo Bayern Munich watamenyana na PSG na Tottenham watawakaribisha AC Milan

Wiki hii imekuwa nzuri kwa Kylian Mbappe, ambaye alivunja rekodi ya mabao PSG kwa bao lake la 201 katika klabu hiyo siku ya Jumamosi

Ni mafanikio makubwa kwa fowadi huyo mwenye umri wa miaka 24Β  lakini sasa leo anapaswa kuibeba PSG katika mchezo dhidi ya Bayern Munich wakiwa tayari wako nyuma kwa bao 1-0 wakipoteza mchezo wa kwanza nyumbani

Mbappe ameshinda mataji yote ya ndani akiwa na PSG isipokuwa Ligi ya Mabingwa

PSG leo watamkosa Neymar ambaye msimu kwa upande wake umemalizika baada ya kupata majeraha ambayo atafanyiwa upasuaji utakaomuweka nje ya uwanja kwa miezi mitatu au zaidi

Ni wazi Mbappe sambamba na Lionel Messi watahitaji kucheza nafasi kubwa zaidi. Lakini ikiwa PSG itatoka kwenye mashindano katika hatua hii ya mapema, itafungua wimbi la uvumi kuhusu hatma ya Mbappe huko Paris

Tottenham hawajashinda mchezo wowote wa mtoano wa Uropa katika mashindano yoyote ya UEFA tangu watinga fainali ya Ligi ya Mabingwa mnamo 2019

Hilo sio jambo pekee ambalo Spurs inakabiliana nalo inapojiandaa kuwakaribisha AC Milan Jumatano usiku.

Imepita muongo mmoja tangu Antonio Conte afuzu kwa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa akiwa kama meneja, na kufuzu hatua ya 16 bora na hatua ya makundi katika kila moja ya kampeni zake nne za mwisho kwenye michuano ya Ulaya

Yawezekana hawatapata nafasi nzuri zaidi ya kufika robo-fainali ya Ligi ya Mabingwa kuliko mwaka huu wanapokutana na timu iliyo katika hali sawa na wao

Wakiwa nyuma kwa bao 1-0, Conte na Spurs wanahitaji kutinga robo fainali mwaka huu kuonyesha timu hii imeimarika kutoka msimu uliopita

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
12m ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
3h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
4h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
4h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
5h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
6h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
7h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
7h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’