Leo majira ya saa 1 usiku katika uwanja wa Benjamin Mkapa, kikosi cha Yanga kitakuwa uwanjani kuikabili Real Bamako katika mchezo wa kombe la Shirikisho barani Afrika
Ni mchezo wa raundi ya nne kundi D Yanga ikizihitaji alama zote tatu ili kuweka hai matumaini ya kutinga robo fainali
Baada ya kufanikiwa kuondoka na alama moja kule Mali, leo Yanga ina kazi moja tu, kuhakikisha inashinda ili kufikisha alama saba
Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amewataka mashabiki wa timu hiyo kuhakikisha wamekata tiketi zao mapema mpaka sasa tiketi za VIP A zikiwa zimemalizika
Kamwe amesema leo wachezaji wanahitaji kuona 'vibe' zaidi ya lile waliloshuhudia katika mchezo dhidi ya TP Mazembe ambayo Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 3-1
Kama Yanga itashinda leo na TP Mazembe kupoteza nchini Tunisia dhidi ys US Monastir, basi Yanga itahitaji kushinda mchezo utakaofuata dhidi ya US Monastir ambao pia utapigwa dimba la Mkapa ili kufuzu robo fainali