PSG - Bayern - AC Milan - Tottenham

Bayern, AC Milan zatinga robo fainali UEFA

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Mar 2023
Bayern, AC Milan zatinga robo fainali UEFA

Bayern Munich imeichapa PSG mabao 2-0 katika mchezo wa mkondo wa pili wa hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, na kutinga robo fainali kwa jumla ya mabao 3-0.

Wafaransa walipata nafasi nzuri ya kusawazisha bao katika kipindi cha kwanza huku Yann Sommer akipoteza mpira kwenye eneo la hatari, lakini Matthijs de Ligt alikuwa imara kwenye mstari wa goli kumzuia Vitinha kufunga.

Eric Maxim Choupo-Moting aliongeza faida ya wenyeji mara mbili katika dakika ya 61.

Ilikuwa ni makosa ya kiungo Marco Verratti katika eneo la hatari ndiyo yaliyomtengenezea Moting nafasi hiyo, na Bayern ilihakikisha inawaadhibu wapinzani wao.

Serge Gnabry alifunga bao la pili kwenye dakika ya 89, akimalizia shambulizi la kushtukiza

Bayern wanatinga hatua ya nane bora kwa msimu wa nne mfululizo, huku PSG wakitolewa katika hatua hii kwa mwaka wa pili mfululizo

Nao AC Milan wametinga robo fainali baada ya matokeo ya suluhu ya bila kufungana dhidi ya Tottenham Hotspurs

AC Milan walishinda bao 1-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa Italia

More Stories

Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
Klopp amchagua ter stegen, kipa namba moja ujerumani
1m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
29m ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
1h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
2h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
3h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
3h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
16h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’