Kikosi cha KMC Fc leo kitashuka katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es salaam kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Kagera Sugar utakaochezwa saa 16 00 jioni
Timu hiyo ya Manispaa ya Kinondoni chini ya kocha Mkuu Thierry Hitimana itawakaribisha Kagera Sugar katika mchezo ambao wanahitaji kushinda ili kujiondoa kwenye hatari ya kuteremka daraja
Kocha Msaidizi wa timu himu hiyo Ahmad Ally amesema kuwa kama benchi la ufundi limefanya maandalizi ya kutosha na kwamba kila mmoja yupo tayari katika mchezo huo na kusisitiza kuwa utakuwa na ushindani mkubwa kutokana na kwamba Kagera Sugar inushindani kwani hata kwenye msimamo wa Ligi wapo kwenye nafasi nzuri.
"Tunakwenda kucheza nyumbani lakini tutakuwa na mechi ngumu kwa kuwa tunapresha ya kukosa matokeo rafiki kwenye michezo yetu iliyopita, Ila tumejipanga kukabiliana na presha hiyo lakini pia kutumia vizuri uwanja wa nyumbani," alisema Kocha Ahmad
KMC leo itashuka uwanjani bila kiungo wake Baraka Majorogo ambaye ni majeruhi



