Kikosi cha Simba kinatarajiwa kuondoka jijini Dar es salaam leo Alhamisi kuelekea Morogoro tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar ambao utapigwa Jumamosi March 11 katika uwanja wa Manungu Complex, Turiani
Meneja wa Habari na mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema wanakwenda mkoani Morogoro wakiwa na kikosi chao kamili, nyota wawili pekee wakibaki jijini Dar es salaam wakiwa ni majeruhi
Ahmed amewataja wachezaji hao ni Kibu Denis na Augustine Okrah ambao wanaendelea na program maalum za mazoezi
Ahmed amesema wamesahau shamrashamra za ushindi dhidi ya Vipers Fc sasa nguvu zao wanazielekeza kwenye ligi wakiwa katika mbio za kuwania ubingwa msimu huu
Simba inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi ikiwa na alama 54 nyuma ya vinara wa ligi hiyo Yanga wenye alama 62