Ligi Kuu ya NBC imeingia raundi ya 25 ambapo leo mchezo mmoja umepigwa kati ya KMC dhidi ya Kagera Sugar
Baada ya kucheza mechi nane pasipo ushindi, hatimaye KMC wamezinduka leo wakipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar
Mabao yote ya KMC yalifungwa na kiungo mshambuliaji Daruweshi Saliboko katika mchezo ambao KMC wanafurahia ushindi tu lakini hawakucheza vizuri sana
Ni matokeo ambayo yamerudisha imani ya kubaki ligi kuu kwa watoza ushuru hao kutoka Manispaa ya Kinondoni
KMC wamepanda mpaka nafasi ya 11 kwenye msimamo wa ligi wakifikisha alama 26