Kocha Stars atizame Ligi za chini pia

Joel JJ By Joel JJ β€’ 10th March 2023


Kocha Stars atizame Ligi za chini pia

Baada ya wiki iliyopita Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kumtangaza Adel Amrouche kuwa kocha mpya wa timu ya taifa ‘Taifa Stars’, beki wa zamani wa Simba na Sigara, Hamis Kondo amemshauri kocha huyo kuwapa nafasi katika timu ya Taifa wachezaji wanaofanya vizuri ligi za chini

Tangu kutimuliwa kwa Kim Poulsen, Agosti 29, mwaka jana, Stars ilikuwa chini ya kocha wa muda Mzambia, Hanour Janza ambaye naye aliamua kurudi kwao baada ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Klabu ya Zesco United.

Amrouche raia wa Ubelgiji mwenye asili ya Algeria, ana uzoefu mkubwa na soka la Afrika baada ya kufundisha klabu na timu za taifa katika ukanda wa Kusini, Mashariki Kati na Kaskazini.

Kocha huyo amewahi kuwa kocha bora wa Afrika Mashariki mwaka 2013 wakati akiinoa na kuipa Kenya 'Harambee Stars' ubingwa wa Cecafa Challenge na kabla ya hapo alifika nusu fainali mara mbili akiwa na kikosi cha Burundi.

Kondo ambaye amewahi pia kuichezea CDA alisema Taifa Stars ni ya wachezaji wote ila sifa ni lazima wawe na uwezo mkubwa bila kuangalia anacheza daraja gani.

"Simba na Yanga lazima azipe kipaumbele katika uteuzi wa timu kwa sababu wachezaji wake wana kiwango bora na wanapata uzoefu wa mashindano ya kimataifa ambayo wanashiriki, lakini lazima awaangalie na wachezaji wa chini kama kwenye Championship wapo baadhi wanaweza"

"Ukiwaweka na wale wanakuwa wanajifunza na baadaye watazidi kuwa wazuri na itakuwa ni hazina kwa Taifa," alisema Kondo

Mwanaspoti


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.