Wakiwa wametoka kujeruhiwa vikali na Liverpool, Mashetani wekundu walisahau machungu ya kipigo na kuiadhibu vikali Real Betis kwenye mchezo wa ligi ya Europa 16 bora
Manchester United iliichabanga Real Betis mabao 4-1 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Old Trafford jana
Mashabiki wa Man United hawakutarajia kuiona timu yao ikiwa katika kiwango bora baada ya kufumuliwa mabao 7-0 na Liverpool siku chache zilizopita kwenye ligi ya Premia

Mkufunzi wa Man United Erik Ten Hag alionyesha kuwa na imani na kikosi chake na hakika pengine wangeweza kumaliza machungu kwenye mchezo huo kwani walitengeneza nafasi nyingi ambazo zingewapa zaidi ya mabao manne
"Muhimu ni vile tunacheza baada ya kupoteza, unaona hii sio mara ya kwanza tunafanya hivi msimu huu," Ten Hag aliiambia BT Sport
"Tayari imekuwa mara tano au sita, tunaweza kujipanga upya na kurejea tukiwa imara, hii ni dalili njema kwetu"



