Simba - Mtibwa Sugar

Robertinho aipania Mtibwa Sugar

Joel JJ By Joel JJ
10 Mar 2023
Robertinho aipania Mtibwa Sugar

Wakiwa wamewasili salama mkoani Morogoro, Kocha Mkuu wa Simba, Roberto Oliviera ‘Robertinho’, amesema anatarajia kutumia mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Mtibwa Sugar itakayochezwa kesho kama sehemu ya maandalizi ya kuwakabili Horoya AC kutoka Guinea

Simba itaikaribisha Horoya AC katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayochezwa Machi 18, mwaka huu kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Robertinho amesema kikosi chake kiko imara na tayari kuzisaka pointi tatu dhidi ya Mtibwa Sugar ili kuendelea kujiweka katika sehemu salama kwenye mbio zao za kuwania ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Kocha huyo alisema anafahamu Mtibwa Sugar ni moja ya timu nzuri hapa nchini, hivyo watacheza kwa umakini mkubwa ili kuhakikisha wanaendelea kujiimarisha kwenye msimamo wa ligi hiyo.

"Kupata pointi tatu kutoka kwa Mtibwa Sugar kutatupa morali kuelekea mechi ijayo ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Horoya AC. Tunataka kuendelea kupata matokeo bora, itatusaidia kujiamini zaidi," alisema kocha huyo

Aliongeza mechi hiyo dhidi ya Mtibwa Sugar itakuwa na ushindani kwa sababu wenyeji wanahitaji kulinda heshima ya kucheza nyumbani na wao wanahitaji kuondoka na pointi tatu muhimu.

"Tunaifahamu Mtibwa Sugar, tunajua haitakuwa mechi rahisi kutokana na ubora walionao hasa kwa sababu watakuwa wanacheza kwenye Uwanja wa nyumbani, tunahitaji matokeo chanya katika mchezo wetu wa Jumamosi"

"Hii mechi itakuwa na mambo mawili, kuhitaji ushindi na kurejea nyumbani na pointi tatu, lakini inawapa wachezaji wangu molari kuelekea mechi yetu ijayo ya kimataifa,” alisema Kocha huyo"

Katika mechi ya kesho, Simba itawakosa nyota wake wanne ambao ni Kibu Denis, Ismael Sawadogo na Augustine Okrah ambao ni majeruhi na kipa chaguo la pili, Beno Kakolanya, ambaye ana ruhusa maalum kwa ajili ya kumaliza matatizo yake ya kifamilia.

More Stories

BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
12m ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
26m ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
1h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
1h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
2h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
4h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
14h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
14h ago
READ MORE →