Nahodha wa Yanga Bakari Nondo Mwamnyeto amejumuishwa katika kikosi cha wiki kwenye michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika baada ya mechi za raundi ya nne
Mwamnyeto alionyesha kiwango bora katika mchezo dhidi ya Real Bamako uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa juzi na Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 2-0
Tangu arejeshwe kwenye kikosi cha kwanza Mwamnyeto amecheza mechi tatu za makundi kombe la Shirikisho dhidi ya TP Mazembe na mechi mbili dhidi ya Real Bamako
Mwamnyeto pia alitumika kwenye mechi ya ligi kuu dhidi ya KMC Yanga ikiibuka na ushindi wa bao 1-0 na kombe la FA dhidi ya Tanzania Prisons uliopigwa uwanja wa Azam Complex, Yanga ikishinda mabao 4-1
Mwamnyeto hakuanza vyema msimu huu akipoteza nafasi yake kwenye kikosi cha kwanza kocha mkuu wa Yanga Nasreddine Nabi akiamua kumrejesha Yannick Bangala kwenye safu ya ulinzi
Ni wazi kiwango chake sasa kimeimarika, kujumuishwa kwenye kikosi cha wiki cha CAF ni ishara ya ubora alionao kwa sasa
