Yanga - Geita Gold

Mechi dhidi ya Geita Gold ni ngumu - Kaze

Joel JJ By Joel JJ
11 Mar 2023
Mechi dhidi ya Geita Gold ni ngumu - Kaze

Kocha Msaidizi wa Yanga Cedric Kaze amesema kikosi kiko tayari kwa mchezo wa ligi kuu dhidi ya Geita Gold ambao utapigwa kesho Jumapili March 12 katika uwanja wa Azam Complex

Kaze amesema wanatambua mechi dhidi ya Geita Gold haijawahi rahisi lakini wamejipanga kushinda mchezo huo ili kuwa kwenye nafasi nzuri ya kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo

"Tunakwenda kucheza mechi ngumu dhidi ya Geita Gold, timu yenye Mwalimu mwenye uzoefu mkubwa na ligi ya Tanzania. Mechi hii haijawahi kuwa rahisi lakini tunapaswa kupambana ili kupata ushindi"

"Tumetoka kucheza mechi ngumu ya Shirikisho dhidi ya Real Bamako, tuna changamoto ya uchovu na fatique lakini tunapaswa kufanya nguvu zote ili kuhakikisha tunashinda na kujiweka katika nafasi nzuri ya kutetea ubingwa wetu," alisema Kaze

Nae mshambuliaji kinara wa mabao ligi kuu ya NBC, FIston Mayele amesema wachezaji watapambana ili kuhakikisha wanatimiza malengo ya kutwaa ubingwa

Mayele amesema yeye binafsi anatamani kuibuka mfungaji bora msimu huu hivyo ataendelea kupambana kwa kushirikiana na wachezaji wenzake kwanza kutimiza malengo ya timu na yake

Mayele ameishukuru klabu ya Yanga kwa kumsaidia kupata nafasi ya kuitwa timu ya Taifa ya DR Congo akiwapa shukrani wadau na mashabiki wa soka nchini ambao wanamuunga mkono

More Stories

SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
3m ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE →