Bournemouth wamejiondoa kwenye eneo la kushuka daraja baada ya kuichapa Liverpool bao 1-0 katika mchezo wa Premia uliopigwa leo
Billing alifunga bao pekee la Bournemouth katika mchezo ambao Mohammed Salah alikosa mkwaju wa penati kwa upande wa Liverpool
Ni kipigo kisichotarajiwa kwa Liverpool ambao wametoka kuifumua Manchester United mabao 7-0 katika mchezo wa ligi uliopita
Bournemouth wamefikisha alama 24 na kupanda mpaka nafasi ya 17 wakati Liverpool wamesalia nafasi ya tano wakiwa na alama 42



