Yanga

Yanga yaichakaza Geita Gold

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Mar 2023
Yanga yaichakaza Geita Gold

Yanga imeendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi kuu ya NBC baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Geita Gold katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi

Geita Gold walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza kwenye dakika ya 20 kupitia kwa Elias Maguli aliyemzidi maarifa mlinzi wa Yanga Dickson Job kabla kuukwamisha mpira kimiani

Kuingia kwa bao hilo kuliiamsha Yanga na kufanya mashambulizi mfululizo kwenye lango la Geita lakini mpaka mapumziko Wananchi walikuwa nyuma kwa bao 1-0

Mabadiliko aliyofanya kocha wa Yanga Nasreddine Nabi kwa kuwaingiza Metacha Mnata, Stephane Aziz Ki na Jesus Moloko nafasi za Djigui Diarra, Mudathir Yahya na Farid Mussa yalikuwa na faida kwa Yanga kwani Wananchi walifanya msako mkali kwenye lango la Geita Gold

Dakika tatu tu zilitosha wao kurejea mchezoni kupitia kwa Kennedy Musonda aliyefunga bao mahiri la kichwa kwenye dakika ya 48 kabla ya Clement Mzize kuongeza bao la pili kwenye dakika ya 50 akimalizia mpira uliotemwa na mlinda lango wa Geita Gold baada ya shuti la Musonda

Msumari wa tatu wa Yanga uliwekwa kimiani na Jesus Moloko kwenye dakika ya 70 baada ya pasi mahiri kutoka kwa Aziz Ki

Ni alama tatu ambazo zimeifanya Yanga ijiimarishe kileleni mwa msimamo wakifikisha alama 65 wakirudisha gap la alama nane dhidi ya Simba

Kimahesabu Yanga inahitaji kushinda mechi tatu zinazofuata (ukiwemo mchezo dhidi ya Simba) ili kutetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
3h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
7h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
7h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
8h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
9h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
10h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
10h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
1d ago
READ MORE β†’