Simba

Simba yataja viingilio mechi dhidi ya Horoya Ac

Joel JJ By Joel JJ
13 Mar 2023
Simba yataja viingilio mechi dhidi ya Horoya Ac

Klabu ya Simba imetangaza viingilio vya mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Horoya Ac ambao utapigwa Jumamosi, March 18 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari, Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema wanahitaji mashabiki wengi wajitokeze dimba la Benjamin Mkapa hivyo hakuna mabadiliko katika viingilio vya mchezo uliopita dhidi ya Vipers Fc

"Mechi hii dhidi ya Horoya Ac tunataka kujaza uwanja wa Benjamin Mkapa, hivyo viingilio ni vilevile, Mzunguuko ni Tsh 3,000/-, VIP C ni Tsh 10,000/-, VIP B ni Tsh 20,000/- na VIP A ni Tsh 30,000/-"

"Pia tutakuwa na tiketi za Executive ambazo gharama yake ni kuanzia Tsh 20,000/- kwa ajili ya makampuni na hata watu binafsi yakiwemo matawi ya Simba. Kwa wale watakaokata tiketi hizi watapatiwa kibaki cha kuingia uwanja wa Mkapa na magari yao"

"Tiketi za Platinum pia zitapatikana kwa Tsh 150,000/- zikiwa na huduma maalum pamoja na kifurushi cha Simba"

"Wapinzani wetu Horoya AC watawasili nchini usiku wa kuamkia Ijumaa, March 17 hivyo kwa wale wanaopenda kwenye kuwapokea taarifa hii iwafikie"

Aidha amesema wameandaa hamasa kubwa katika mji wa Dar es salaam ili kuhakikisha wanaujaza uwanja wa Benjamin Mkapa siku ya Jumamosi

"Tangu kuanza kwa michuano ya ligi ya mabingwa msimu huu hatujaweza kujaza uwanja, lakini kwenye mchezo dhidi ya Horoya AC tunataka kujaza uwanja wa Benjamin Mkapa. Hawa Horoya pamoja na ukubwa wao, tukiwapigia kelele hawatatoka salama," alisema Ahmed

More Stories

SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
1m ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE →
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE →
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE →
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE →