Kiungo wa Manchester United Casemiro anatazamiwa kukabiliwa na adhabu nyingine baada ya kupokea kadi nyekundu dhidi ya Southampton hapo jana
Alipewa kadi ya njano na mwamuzi baada ya kumzonga Carlos Alcaraz. Lakini uamuzi huo ulipitiwa na VAR na akapewa kadi nyekundu
Hii ni kadi nyekundu ya pili kwa Mbrazil huyo msimu huu baada ya kupata kadi nyekundu ya moja kwa moja dhidi ya Crystal Palace mnamo Februari
Mechi hii ilikuwa mechi ya pili ya Casemiro Ligi Kuu tangu kutumikia adhabu hiyo ya awali
Casemiro sasa atakabiliwa na adhabu ya kutocheza mechi nne kutokana na kadi nyekundu hiyo
Hii ni kwa sababu ni kadi yake nyekundu ya pili msimu huu, hivyo adhabu ya awali ya mechi tatu inaongezwa hadi nne.
Kufungiwa kwa kadi nyekundu hufanywa kupitia mashindano yote ya ndani, kwa hivyo itatumika kwa mechi zijazo za Kombe la FA na Ligi Kuu
Mechi atakazokosa nu dhidi ya Fulham (H), Newcastle (A), Brentford (H) na Everton (H)



