Mapema leo, mshambuliaji wa Yanga Kennedy Musonda amepokea zawadi ya medali kutoka kwa mtoto Lucas Gomez Usoz raia wa Hispania
Kijana huyo mwenye umri wa miaka 8 anayeishi jiji la Madrid, alituma Medali hiyo kupitia ubalozi wa Hispania hapa Tanzania
Musonda amekabidhiwa medali hiyo leo na Balozi Jorge Moragas mbele ya Rais wa Yanga Injinia Hersi Said
Gomez alivutiwa na uchezaji wa Musonda wakati akiitumikia klabu yake ya zamani ya Power Dynamos FC ya nchini Zambia.
Hafla hiyo fupi iliyoandaliwa na balozi ilifanyika kwenye makazi yake eneo la Oyster bay, jijini Dar es salaam




