Juventus

Pogba majanga Juventus

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Mar 2023
Pogba majanga Juventus

Kiungo wa Juventus, Paul Pogba anatarajiwa kuwa nje kwa angalau wiki tatu baada ya kuumia

Pogba (29) atakosa nafasi ya kujumishwa kwenye kikosi cha Ufaransa kwa ajili ya kuwania kufuzu kwa Euro 2024.

Pogba hakujumuishwa kwenye kikosi cha Juventus kilichocheza na Freiburg wiki iliyopita, pia alikosa mechi ya ushindi wa 4-2 dhidi ya Sampdoria Jumapili

"Leo asubuhi Pogba alikuwa akipiga faulo akahisi maumivu katika paja lake," kocha wa Juve Massimiliano Allegri alisema baada ya mechi ya Jumapili

Taarifa ya klabu ilisema kuwa Pogba alifanyiwa vipimo vya afya siku ya Jumatatu na kwamba amepata majeraha kidogo kwenye paja lake la mguu wa kulia

"Tayari ameanza mchakato wa matibabu ili kuhakikisha anarejea haraka katika majukumu yake," aliongeza Allegri

Juventus wana mchezo wa marudiano dhidi ya Freiburg siku ya Alhamisi, huku Pogba akikosa mchezo wa kwanza baada ya kuchelewa kuungana na timu Jumatano iliyopita

Pogba amecheza mechi mbili pekee akitokea benchi tangu ajiunge tena na Juve kutoka Manchester United msimu uliopita wa joto, huku mechi ya kwanza akicheza Februari 28.

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’