Ligi ya Mabingwa Ulaya wiki hii

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th March 2023


Ligi ya Mabingwa Ulaya wiki hii

Mikiki mikiki ya kusaka nafasi ya kutinga robo fainali ya ligi ya mabingwa barani ulaya inaendelea leo kwa mechi mbili kupigwa

Manchester City ambao walilazimishwa sare ya bao 1-1 katikc mchezo wa kwanza dhidi ya RB Leipzig uliopigwa Ujerumani, leo wanahitaji kushinda nyumbani ili kutinga robo fainali

Kwa Kocha Pep Guardiola, michuano hii ina umuhimu mkubwa kwake kwani ndio michuano pekee ambayo hajaweza kushinda tangu atue Manchester City

Guardiola ana rekodi mbaya na ligi ya mabingwa kwani tangu alipotwaa taji hilo akiwa na Fc Barcelona mara mbili, hajawahi kushinda tena

Mechi nyingine ni kati ya Porto dhidi ya Inter Milan ambapo wenyeji Porto watahitaji kupindua matokeo ya kuchapwa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza uliopigwa Italia

Kesho Napoli itachuana na Entracht Frankfurt, wababe hao wa Italia wakiwa mbele kwa mabao 2-0 na mcheo mwingine ni kati ya Real Madrid dhidi ya Liverpool

Madrid wako mbele kwa ushindi wa mabao 5-2 ugenini, wanahitaji matokeo yoyote isipokuwa kufungwa zaidi ya tofauti ya mabao matatu ili waweze kufuzu robo fainali


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.