Arteta afurahia urejeo wa Jesus

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th March 2023


Arteta afurahia urejeo wa Jesus

Arsenal hawana muda wa kupumzika kulingana na vile ratiba ya mechi zao ilivyo

Kikosi cha Mikel Arteta kilicheza mechi nyingi katika mwezi uliopita na bado kinaweza kukabiliana na michezo mingine 17 kabla ya mwisho wa msimu

The Gunners wanaweza kutwaa taji la Premia  na kombe la Uropa kwa mara ya ppili

Yatakuwa mafanikio makubwa kwa Arsenal msimu huu, lakini bado kuna mechi nyingi za kucheza

Ushindi wa 3-0 wa Jumapili dhidi ya Fulham ulimaanisha Arsenal kurejea uongozi wao wa pointi tano kileleni mwa Ligi ya Premia.

Kurejea kwa Gabriel Jesus baada ya miezi mitatu nje ya uwanja, kulimpatia Arteta imani mpya

 "Kaongeza nguvu, ni mechi yake ya kwanza leo baada ya muda mrefu. Hatukujua kama ulikuwa mchezo sahihi leo," Arteta alikiri baada ya mchezo.

“Aliniambia siku chache zilizopita 'bado sijawa sawa' lakini jana akaniambia 'nipo tayari' nikasema sawa tukapata fursa ya kumpa nafasi"

"Ni hatua ya kwanza ya kumpa nguvu kubwa. Anaonekana kuwa huru, anaonekana tayari na mara moja alitengeneza nafasi hizo mbili kubwa. Ni vyema kuwa naye tena," alisema Arteta

Mchezo wa marudiano wa hatua ya 16 bora wa Ligi ya Europa Alhamisi dhidi ya Sporting CP unatoa fursa nzuri kwa Arteta kutoa dakika zaidi kwa ajili ya Jesus.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 alishiriki kwa dakika 13 katika Craven Cottage na anaweza kupata dakika nyingi zaidi katika mchezo ujao

Wachezaji watatu ambao walikosa sare ya wiki iliyopita mjini Lisbon wote walirejea uwanjani haraka. Martin Odegaard na Kieran Tierney walikosa mechi ya kwanza kutokana na ugonjwa huku Leandro Trossard akiwa mchezaji wa kwanza kutoa pasi tatu za mabao katika kipindi cha kwanza cha mchezo wa ugenini katika historia ya Ligi Kuu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.