Erling Haaland alisawazisha rekodi ya Ligi ya Mabingwa kwa kufunga mabao matano na kuifanya Manchester City kutinga robo fainali mbele ya RB Leipzig kwa ushindi wa mabao 7-0 kwa mabingwa hao wa Uingereza na kupata ushindi wa jumla wa 8-1 Jumanne usiku
Haaland pia aliweka rekodi mpya ya klabu ya kufunga mabao 39 katika msimu huku vijana wa Pep Guardiola wakifika hatua ya nane bora kwa msimu wa sita mfululizo
City bado hawajashinda taji la Ligi ya Mabingwa, lakini hawajawahi kuwa na mshambuliaji wa ubora wa Haaland kuleta mabadiliko katika hatua za mwisho hapo awali
Akiwa na umri wa miaka 22 sasa ana mabao 33 katika mechi 25 alizocheza kwenye mashindano ya vilabu barani Ulaya
"Nguvu yangu kubwa ni kufunga mabao, mbinu ni kuwa na haraka akilini na kujaribu kuweka mpira mahali ambapo kipa hayupo," alisema Haaland
"Ninajivunia kucheza katika shindano hili, nalipenda, Mabao matano! Kushinda 7-0 ni ajabu!"



