Mashabiki Mbeya City wamjia juu kocha

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th March 2023


Mashabiki Mbeya City wamjia juu kocha

Baaada ya kuambulia kipigo cha mabao 1-2 nyumbani kutoka kwa Ruvu Shooting, mashabiki wa Mbeya City wamemjia juu kocha wao, Mubiru Abdallah

Mbeya City wanasuasua kwenye ligi msimu huu hali inayowafanya kuwa kwenye hatari ya kuingia katika janga la kushuka daraja licha ya kushika nafasi ya kumi

Wagonga nyundo hao wa Jiji la Mbeya, wamejikusanyia alama 27 katika michezo 25 waliyocheza, bado michezo mitano kumaliza msimu huu

"Kocha anazingua sana na mbinu zake zimefeli kabisa maana unaona timu haina uwezo kabisa wa kupambana tofauti na msimu uliyopita," alisema mmoja wa mashabiki hao

Mbeya City katika michezo mitano iliyosalia, mitatu itacheza ugenini dhidi ya Namungo FC, Kagera Sugar na Geita Gold


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.