Droo ya robo fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) imefanyika leo ambapo mabingwa watetezi Yanga wamepangwa kuchuana na Geita Gold katika mchezo utakaopigwa jijini Dar es salaam
Katika droo hiyo pia imeshuhudia klabu ya Simba ikipangwa dhidi ya Ihefu Fc wakati Azam Fc wakipangwa kuchuana na Mtibwa Sugar huku Singida Big Stars wakiumana na Mbeya City
Aidha, TFF wameweka hadharani viwanja ambavyo mechi za nusu fainali na fainali zitapigwa
Nusu fainali ya kwanza itachezwa uwanja wa Nangwanda Sijaona (Mtwara) na nusu fainali ya pili uwanja wa Liti (Singida). Fainali itachezwa katika uwanja wa Mkwakwani (Tanga).
Kwenye nusu fainali, Mshindi wa mchezo kati ya Yanga dhidi ya Geita Gold atachuana na mshindi wa mchezo kati ya Singida BS dhidi ya Mbeya City uwanja wa Liti
Wakati mshindi wa mchezo kati ya Simba dhidi ya Ihefu Fc atachuana na mshindi wa mchezo kati ya Azam Fc dhidi ya Mtibwa Sugar uwanja wa Nangwanda Sijaona
Mechi za robo fainali zitapigwa kati ya April 01-06 2023



