Mwanamuziki Lokassa ya MBongo afariki Dunia

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th March 2023


Mwanamuziki Lokassa ya MBongo afariki Dunia

Mkongwe wa kupiga gitaa la rhythm kutoka nchini DR Congo, Lokassa Kasia Dennis maarufu Ya M'Bongo amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 76, baada ya kuugua kwa muda mrefu nchini Marekani

Lokassa ambaye alikwa kiongozi wa bendi maarufu ya Soukous Stars, alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari.

Kwa mujibu wa mtandao wa The Standard wa nchini Kenya, taarifa ya promota wa muziki wa Congo anayeishi Nairobi, Tabu Osusa, Ya Mbongo alikuwa akiugua magonjwa yanayohusiana na moyo.

Lokassa atakumbukwa kwa nyimbo nzuri ambazo alishiriki kuziandaa na kupiga gitaa kama Bonne Annee, Monica, Marie-Josse na Assitou


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.