Mshambuliaji kinda wa Manchester City Erling Haaland ametamba kuwa alisajiliwa na timu hiyo ili kuwasaidia kushinda Ligi ya Mabingwa kwa sababu tayari wanajua jinsi ya kushinda Ligi ya Premia.
Haaland, 22, jana alifunga mabao matano katika ushindi wa 7-0 wa City dhidi ya RB Leipzig na kujihakikishia nafasi ya kufuzu kwa robo fainali ya Ligi ya Mabingwa
Manchester City wanalisaka taji la kwanza mafanikio yao makubwa ikiwa ni kumaliza nafasi ya pili mwaka 2021 wakifungwa kwenye fainali na Chelsea Fc
"Bila shaka klabu inataka kushinda Ligi ya Mabingwa. Wameshinda mataji manne kati ya matano ya mwisho ya Ligi Kuu. Hawakunileta kushinda Ligi Kuu kwa sababu tayari wanajua jinsi ya kushinda"
"Kwa hivyo, unaweza kusoma niko hapa kujaribu kusaidia klabu kujiendeleza zaidi na kushinda Ligi ya Mabingwa kwa mara ya kwanza," alisema Haaland
Manchester City wameshinda mataji 17 tangu Sheikh Mansour achukue klabu hiyo mwaka 2008, yakiwemo mataji sita ya Ligi Kuu ya Uingereza, manne kati ya hayo yamepatikana baada ya Pep Guardiola kuteuliwa mwaka 2016.