Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi March 16 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
16 Mar 2023
Tetesi za soka Ulaya, Alhamisi March 16 2023

Mshambuliaji wa Argentina Lionel Messi, 35, atapewa ofa ya euro milioni 220 (£193m) kwa mwaka ili kuhamia klabu ya Saudi Arabia mkataba wake wa Paris St-Germain utakapokamilika msimu wa joto. (Marca kwa Kihispania)

Mshambulizi wa Manchester City Julian Alvarez, 23, anatazamiwa kusaini mkataba mpya ambao utamweka mshindi huyo wa Kombe la Dunia la Argentina Etihad hadi 2028. (Mail).

Kiungo wa kati wa Ufaransa Paul Pogba anataka kusalia Juventus msimu ujao, licha ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 kucheza kwa dakika 35 tu kwenye ligi ya Serie A msimu huu kwa sababu ya majeraha. (90 Min)

Meneja wa Barcelona Xavi Hernandez tayari amezungumza na kiungo wa kati wa Ujerumani Ilkay Gundogan, 32, kuhusu uhamisho. Mkataba wa Gundogan huko Manchester City unamalizika majira ya joto. (AS - kwa Kihispania)

Borussia Dortmund huenda ikampa winga wa kimataifa wa Ujerumani Julian Brandt, 26, kandarasi mpya katika jitihada za kuzuia nia ya Arsenal na Tottenham. (Bild ya Michezo - kwa Kijerumani)

Manchester United wanaweza kuwasilisha ofa ya pauni milioni 105 kumnunua mshambuliaji wa Eintracht Frankfurt na Ufaransa Randal Kolo Muani, 24. (Sport Bild - kwa Kijerumani)

Chelsea wana nia ya kumsajili Manu Kone wa Borussia Monchengladbach huku kiungo huyo wa kati wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 21 akivutia pia Paris St-Germain. (Sun)

The Blues wako tayari kumuuza kiungo wa kati wa kimataifa wa Uingereza Ruben Loftus-Cheek, 27, msimu huu wa joto na klabu tano za Premier League, pamoja na AC Milan na Roma zinazowania. (Football Insider)

Mshambulizi wa Ufaransa Karim Benzema, 35, ameripotiwa kukubali kusaini mkataba mpya na Real Madrid. (L'Equipe - kwa Kifaransa)

West Ham wanatazamia kumnunua mshambuliaji wa Werder Bremen na Ujerumani Niclas Fullkrug, 30. (Sport Bild via Sport Witness)

Newcastle, Aston Villa, Wolves na Leeds wana nia ya kumsajili beki wa pembeni wa kimataifa wa Ureno Raphael Guerreiro, 29, mkataba wake na Borussia Dortmund utakapokamilika msimu wa joto. (Dakika 90)

Fulham wanamfuatilia kiungo Mfaransa Edouard Michut, 20, ambaye kwa sasa yuko kwa mkopo Sunderland kutoka Paris St-Germain. (Fabrizio Romano)

BBC

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
35m ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
11h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
19h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
19h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’