Arsenal yapigwa kumbo Europa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th March 2023


Arsenal yapigwa kumbo Europa

Usiku wa kuamkia leo Arsenal iliondoshwa kwenye ligi ya Europa kwa mikwaju ya penati 5-3 baada ya matokeo ya sare ya bao 1-1 katika mchezo uliopigwa kwa dakika 120

Changamoto ya mikwaju ya penati ilitumika kupata mshindi baada ya matokeo ya jumla kuwa 3-3. Timu hizo zilitoka 2-2 kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa Ureno

Granit Xhaka aiitanguliza Arsenal mapema lakini shuti la mbali la Pedro Goncalves liliirejesha Sporting mchezoni na kulazimisha dakika 30 za muda wa ziada

Kocha Mkuu wa Arsenal Mikel Arteta alifanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake akiwapa mapumziko wachezaji wake muhimu

Arsenal imeweka nguvu kubwa kwenye kuwania ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza ambapo siku ya Jumapili watachuana na majirani zao kutoka jiji la London, Crystal Palace

Katika mechi nyingine Manchester United ilitinga robo fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-1 dhidi ya Real Betis

Man United walishinda 4-1 kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa Uingereza

Timu nyingine zilizotinga robo fainali ni Fayenoord, Sevilla, Juventus, B Leverkusen, Roma na Union St Gilloise


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.