Simba

Robertinho apania ushindi dhidi ya Horoya Ac

Joel JJ By Joel JJ
17 Mar 2023
Robertinho apania ushindi dhidi ya Horoya Ac

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema maandalizi kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Horoya AC, yamekamilika

Robertinho amesema wachezaji wake wanatambua umuhimu wa mchezo huo ambao wanahitaji kushinda ili kutinga robo fainali

"Tunawaheshimu wapinzani wetu lakini tuna nafasi kubwa ya kufanya vizuri mbele ya mashabiki wetu hapo kesho"

"Tulicheza vizuri mchezo wa kwanza lakini hatukutumia vyema nafasi tulizotengeneza lakini tumefanyia kazi mapungufu kuona tunafanya vizuri zaidi"

"Haikuwa rahisi kushinda mechi mbili dhidi ya Vipers Fc lakini wachezaji wetu walipambana, naamini siku ya kesho tutakuwa na wakati mzuri pia"

"Tunataka kucheza vizuri na kushinda, hii ni mechi kubwa tunapaswa kujitolea kwa ari kubwa, tunataka kushinda mchezo huu"

"Tunapaswa kucheza vyema tunapokuwa na mpira lakini pia hata pale bila ya mpira kwani tutakutana na nyakati zote hizi"

"Siwezi kuweka hadharani mbinu na kikosi nitakachotumia hapo kesho lakini nawahakikishia tuna timu imara, wachezaji wote wako tayari kwa mchezo huu muhimu," alisema Robertinho

Nae nahodha msaidizi wa Simba Shomari Kapombe amesema wamekamilisha maandalizi kuelekea mchezo huo na wana matumaini kuwa watapata matokeo mazuri

"Tunajua mechi haitakuwa nyepesi, lakini pia tunajua hii ni mechi muhimu sio kwa Simba tu, bali kwa nchi hivyo wachezaji tuko tayari, muhimu tunawahitaji mashabiki wetu waje kwa wingi, tunawaahidi kupata ushindi," alisema Kapombe

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
5h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
6h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
8h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
8h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
9h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
9h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
9h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
9h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
10h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
12h ago
READ MORE →