Wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika, Simba leo wanatupa karata muhimu uwanja wa Benjamin Mkapa katika mchezo dhidi ya Horoya Ac
Ni mchezo muhimu kwa Simba kuisaka tiketi ya kutinga robo fainali, ushindi wa aina yoyote utawahakikishia Wekundu wa Msimbazi kutinga robo fainali ya tatu katika kipindi cha miaka mitano iliyopita
Hautakuwa mchezo mwepesi kwa kuwa kila timu ina nafasi ya kusonga mbele kama itapata matokeo mazuri
Horoya Ac wanaweza kufurahia alama moja wakifahamu mechi yao ya mwisho wako nyumbani dhidi ya Vipers Fc wakati Simba itasafiri Morocco kuhitimisha hatua ya makundi kwa mchezo dhidi ya wababe Raja Casablanca
Silaha kubwa ya Simba katika mchezo wa leo ni mashabiki wake. Matarajio ni kuwa mashabiki 60,000 watajitokeza kuwaongezea hamasa wachezaji wao
Mkufunzi wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari, ari na morali ya wachezaji iko juu na wana matumaini makubwa ya kushinda mchezo wa leo



