Simba yaifumua Horoya Ac 7-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 18th March 2023


Simba yaifumua Horoya Ac 7-0

Simba inakwenda robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kibabe kabisa kwa ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Horoya Ac katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Hizi ni salamu kwa vigogo wote Afrika kuwa Simba iko tayari kushindania ubingwa msimu huu

Mnyama alianza kampeni yake taratibu kwa kupoteza mechi mbili za kwanza lakini leo anakwenda robo fainali kwa ushindi mkubwa zaidi katika michuano hiyo msimu huu

Ilikuwa siku nzuri kwa Clatous Chama 'Mwamba wa Lusaka' ambaye leo ameondoka na mpira akifunga mabao matatu

Sadio Kanoute leo amewaonyesha kuwa yeye sio kukata umeme tu, hata kufunga anaweza, akiweka kambani mabao mawili yote akimtungua mlinda lango kutoka nje ya 18

Jean Baleke katika ubora mkubwa kabisa akaweka kambani mabao mawili pia sasa akifunga mabao matano katika mechi mbili

Ilikuwa mechi ya upande mmoja, Simba walitawala na pengine Horoya Ac wangeondoka na nyingi zaidi

Kwa hakika Simba sasa iko tayari kutimiza malengo yake ya angalau kucheza nusu fainali ya michuano hiyo msimu huu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.