Simba

Simba yaifumua Horoya Ac 7-0

Joel JJ By Joel JJ
β€’
18 Mar 2023
Simba yaifumua Horoya Ac 7-0

Simba inakwenda robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika kibabe kabisa kwa ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya Horoya Ac katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Hizi ni salamu kwa vigogo wote Afrika kuwa Simba iko tayari kushindania ubingwa msimu huu

Mnyama alianza kampeni yake taratibu kwa kupoteza mechi mbili za kwanza lakini leo anakwenda robo fainali kwa ushindi mkubwa zaidi katika michuano hiyo msimu huu

Ilikuwa siku nzuri kwa Clatous Chama 'Mwamba wa Lusaka' ambaye leo ameondoka na mpira akifunga mabao matatu

Sadio Kanoute leo amewaonyesha kuwa yeye sio kukata umeme tu, hata kufunga anaweza, akiweka kambani mabao mawili yote akimtungua mlinda lango kutoka nje ya 18

Jean Baleke katika ubora mkubwa kabisa akaweka kambani mabao mawili pia sasa akifunga mabao matano katika mechi mbili

Ilikuwa mechi ya upande mmoja, Simba walitawala na pengine Horoya Ac wangeondoka na nyingi zaidi

Kwa hakika Simba sasa iko tayari kutimiza malengo yake ya angalau kucheza nusu fainali ya michuano hiyo msimu huu

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
7h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
7h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
11h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
15h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
17h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
18h ago
READ MORE β†’