Transfer

Tetesi za soka Ulaya, Jumanne March 21 2023

Joel JJ By Joel JJ
β€’
21 Mar 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumanne March 21 2023

Spurs wanataka pauni milioni 100 mbele kwa mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane ikiwa watafikiria kumuuza mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 msimu wa joto wakati atakuwa amebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake. (Times - subscription required)

Manchester City wanazidi kujiamini kuwa wanaweza kumpata Muingereza Jude Bellingham, 19, msimu wa joto, lakini Real Madrid wanasalia kwenye mbio za kumnunua kiungo wa kati wa Borussia Dortmund. (ESPN)

Mtu mwenye nia ya kuinunua Manchester United Sir Jim Ratcliffe anasema hataki kulipa "bei ya kijinga" kwa klabu hiyo. (Wall Street Journal)

Tottenham Hotspur wanatarajiwa kukubaliana na kuondoka kwa meneja wao Muitaliano Antonio Conte, 53, wiki hii, huku mchezaji wa zamani na kocha wa kikosi cha kwanza Mwingereza Ryan Mason, 31, akitarajiwa kuchukua usukani hadi mwisho wa msimu. (Telegraph - subscription required)

Arsenal wako tayari kumpa mchezaji wa Norway Martin Odegaard, 24, mkataba mpya wa kumuweka katika klabu hiyo hadi 2030. (Football Transfers)

Newcastle United inalenga kumlenga kiungo wa Manchester United Scott McTominay msimu huu wa joto na mchezaji huyo wa kimataifa wa Scotland, 26, anaaminika kuwa tayari kuhama. (Telegraph - subscription required)

Matumaini ya Juventus kumsaini N'Golo Kante, 31, bila malipo msimu wa joto yamekatizwa, huku kiungo huyo wa kati wa Ufaransa akitarajiwa kusaini mkataba mpya wa miaka miwili na Chelsea. (Tuttomercato - in Italian)

Arsenal, Tottenham na West Ham wamemtazama mshambuliaji wa Red Bull Salzburg, Noah Okafor, huku kandarasi ya mchezaji huyo wa kimataifa wa Uswizi ikikamilika msimu wa joto 2024. (Mail)

Kipa wa Aston Villa aliyeshinda Kombe la Dunia Emiliano Martinez anasisitiza kuwa anapanga kusalia katika klabu hiyo, licha ya kuvutiwa sana na mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 30. (Mirror)

Chelsea wako tayari kumuuza mlinda mlango wa Senegal Edouard Mendy, 31, kufuatia kuvunjika kwa mazungumzo ya kuongeza mkataba. (Football Insider)

Mchezaji wa Fulham ambaye ni kiungo wa kati wa zamani wa Manchester United Andreas Pereira, 27, anavutia Chelsea, ambao wanamwona Mbrazil huyo kama mbadala wa Muingereza Mason Mount, 24 - lakini wanakabiliwa na ushindani kutoka kwa Atletico Madrid na Paris St-Germain. (ESPN)

Nahodha wa Barcelona Mhispania Sergio Busquets, 34, anafikiria ofa kutoka kwa Ligi Kuu ya Soka na Saudi Arabia, lakini ataamua wakati wa mapumziko ya kimataifa ikiwa atazikataa na kukubali mkataba mpya wa kusalia Nou Camp. (Mundo Deportivo - in Spanish)

BBC

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
11h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
15h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
19h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
21h ago
READ MORE β†’